Kwanza nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujalia
uzima mpaka kufika na kuiona siku hii ya leo.
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, tunayo adhimisha tarehe 8 Machi ya kila mwaka. Kwa mwaka huu kama ilivyo kawaida yetu Watanzania tunaungana na nchi nyingine wanachama wa Umoja wa Mataifa kuadhimisha siku hii Jumatano tarehe 8 Machi, 2017.
Vuguvugu la Siku ya Wanawake
lilianza mwanzoni mwa miaka ya 1900 kupitia kwa wanawake wafanyakazi wa
sekta ya viwanda nchini Marekani walioandamana kupinga mazingira duni ya
kazi zao, walilalamikia ukosefu wa huduma za kijamii na kuwepo kwa
vitendo vya unyanyasaji katika ajira. Kutokana na hali hiyo, nchi ya
Marekani ilikubali kuwa na siku ya maadhimisho ya kitaifa ili kutafakari
masuala mbalimbali yanayohusu haki na ustawi wa wanawake.
Hatimaye Umoja wa Mataifa ulipoanzishwa mwaka 1945; tarehe 8 Machi iliridhiwa kuwa Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani. Uamuzi huo wa Umoja wa Mataifa ulitokana na kukubali kwake kwamba masuala ya haki, maendeleo na usawa wa wanawake yalihitaji msukumo maalumu na wa pekee.
Madhumuni ya kuadhimisho ya Siku
ya Wanawake Duniani ni kuwezesha jamii kupima utekelezaji wa maazimio,
matamko, mikataba na itifaki mbalimbali za Kimataifa/ kikanda na
kitaifa zinazohusu masuala ya maendeleo ya jinsia na wanawake katika
kuhakikisha haki za wanawake kiuchumi, kijamii, na kisiasa zinapatikana
na zinalidwa.
Aidha, madhumuni mahususi ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ni kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kutambua na kuthamini uwezo na mchango mkubwa wa wanawake katika kuleta maendeleo, kuelezea jitihada mbalimbali zilizofanywa na Serikali na wadau wengine katika kuwajengea uwezo wa kiuchumi na kijamii ili waweze kushiriki kikamilifu kujiletea maendeleo yao, familia zao na Taifa kwa ujumla.
Tanzania ilianza kuadhimisha Siku
ya Wanawake Duniani mwaka 1996, maadhimisho yamekuwa yakiandaliwa
Kitaifa na katika ngazi ya mkoa.
Aidha, nikumbushe kwamba katika maadhimisho ya mwaka 2005 Serikali iliweka utaratibu wa kuandaa Maadhimisho ya Kitaifa kila baada ya miaka minne; ili kutoa fursa maalum kwa mikoa, wilaya na wadau wengine kupima mafanikio yaliyofikiwa katika kumwendeleza mwanamke katika ngazi hizo kwa miaka hiyo na ifikapo mwaka wa tano maadhimisho yafanyike kitaifa kwa kutoa taarifa ya utekelezaji kwa nchi nzima.
Mwaka huu kwa Dar es salaam mkuu wa mkoa huo,Paul Makonda ndiye mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yanayofanyika , katika uwanja wa Mwembeyanga Temeke Jijini Dar es Salaam,ila anawakilishwa na mkuu wa wilaya ya Temeke
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu isemayo “Tanzania ya viwanda, Wanawake ndio Msingi wa Mabadiliko ya Kiuchumi”.
Kauli mbiu hiyo inalenga kuikumbusha jamii kuhusu umuhimu wa kujenga mazingira wezeshi kwa Wanawake hasa kutambua mchango wao katika kuleta Maendeleo yao na ya jamii kwa ujumla.
Taarifa hiyo pia imeikumbusha jamii kuhusu wajibu wake ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha, kuwaamini na kuwapa Wanawake haki sawa katika nafasi za Elimu, Uchumi na uongozi ili wawe chachu ya mabadiliko yenye lengo la kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
MWISHO niseme hongera Wanawake wote dunia kwa siku hii muhimu ....wasalaam
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, tunayo adhimisha tarehe 8 Machi ya kila mwaka. Kwa mwaka huu kama ilivyo kawaida yetu Watanzania tunaungana na nchi nyingine wanachama wa Umoja wa Mataifa kuadhimisha siku hii Jumatano tarehe 8 Machi, 2017.
CHIMBUKO LA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI
Hatimaye Umoja wa Mataifa ulipoanzishwa mwaka 1945; tarehe 8 Machi iliridhiwa kuwa Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani. Uamuzi huo wa Umoja wa Mataifa ulitokana na kukubali kwake kwamba masuala ya haki, maendeleo na usawa wa wanawake yalihitaji msukumo maalumu na wa pekee.
MADHUMUNI YA MAADHIMISHO
Aidha, madhumuni mahususi ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ni kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kutambua na kuthamini uwezo na mchango mkubwa wa wanawake katika kuleta maendeleo, kuelezea jitihada mbalimbali zilizofanywa na Serikali na wadau wengine katika kuwajengea uwezo wa kiuchumi na kijamii ili waweze kushiriki kikamilifu kujiletea maendeleo yao, familia zao na Taifa kwa ujumla.
UTARATIBU WA MAADHIMISHO
Aidha, nikumbushe kwamba katika maadhimisho ya mwaka 2005 Serikali iliweka utaratibu wa kuandaa Maadhimisho ya Kitaifa kila baada ya miaka minne; ili kutoa fursa maalum kwa mikoa, wilaya na wadau wengine kupima mafanikio yaliyofikiwa katika kumwendeleza mwanamke katika ngazi hizo kwa miaka hiyo na ifikapo mwaka wa tano maadhimisho yafanyike kitaifa kwa kutoa taarifa ya utekelezaji kwa nchi nzima.
Mwaka huu kwa Dar es salaam mkuu wa mkoa huo,Paul Makonda ndiye mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yanayofanyika , katika uwanja wa Mwembeyanga Temeke Jijini Dar es Salaam,ila anawakilishwa na mkuu wa wilaya ya Temeke
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu isemayo “Tanzania ya viwanda, Wanawake ndio Msingi wa Mabadiliko ya Kiuchumi”.
Kauli mbiu hiyo inalenga kuikumbusha jamii kuhusu umuhimu wa kujenga mazingira wezeshi kwa Wanawake hasa kutambua mchango wao katika kuleta Maendeleo yao na ya jamii kwa ujumla.
Taarifa hiyo pia imeikumbusha jamii kuhusu wajibu wake ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha, kuwaamini na kuwapa Wanawake haki sawa katika nafasi za Elimu, Uchumi na uongozi ili wawe chachu ya mabadiliko yenye lengo la kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
MWISHO niseme hongera Wanawake wote dunia kwa siku hii muhimu ....wasalaam




No comments:
Post a Comment